amreezle

amreezle

Wednesday, June 13, 2012

Another value woman in Africa


Nneka Lucia Egbuna (born 24 December 1980) is a Nigerian-German hip hop/soul singer and songwriter. She sings in both English and Igbo. Nneka is the daughter of an Anambra state- Igbo Nigerian father and a German mother. She was born and raised in Warri, in the Delta region of Nigeria, and went to the primary school of the Delta Steel Company, then the secondary school at the Nigerian National Petroleum Corporation. Nneka relished the experience of singing from an early age in her school and in the church choir. After relocating to Hamburg, Germany, at the age of 18, she pursued a career in singing alongside a degree in Anthropology. She now divides her time between Nigeria and Hamburg.
 This is Official  video its clld  (DO YOU  LOVE ME NOW).JUST VISIT  nneka on facebook also tweeter.
 

miss kuch kuch in africa

Joy Odiete, popularly known as JODIE, born on the 22nd of June, is a young soulful singer from Nigeria with a personality that exudes African freshness and originality.

Being one the favorite finalists in the premier edition of Idols, West Africa, her debut has been anticipated by fans not only in Nigeria, but among other African viewers.
Finally, her first singles, “Kuchi Kuchi” and “Fighter” are out. “Fighter” was born out of her determination to achieve her musical dream and never give up, while “Kuchi Kuchi” is a simple, soothing and rhythmic track inspired by the love of a child.
Jodie is a singer, songwriter and jewelry artiste. She loves being African and so keeps her virgin hair… Jodie is simply “Jodie”! Nigeria]

J’odie, releases her first video, for the baby-inspired Zouk song which was released at the tail end of 2010. The song exudes innocence and is extremely melodic in its delivery and her style can be described in three words; Soulful, Artsy… Simply African.

Sunday, June 3, 2012

Bongo Star Search: Shindano linalotoa washindi wasiomudu ushindani wa muziki


Mwaka huu Bongo Star Search imekuja na kasi mpya. Ikiwa na wadhamini wapya sasa hivi inajulikana kama Epiq BSS. Udhamini huo mnono unaambatana na kitita cha shilingi milioni 50 zitakazotolewa kwa mshindi wa mwaka huu.
Harufu inayodhihirisha kuwa mashindano ya mwaka huu yanaweza kuwa na utofauti mkubwa imeshaanza kunukia. Kwanza kwa matangazo yanayovutia yaliyoandaliwa na wadhamini, yanayosikika kwenye vituo vya radio na kuamsha hamu ya watazamaji wa TV wanayoyasubiria. Continue reading

Evander Holyfield kwenda jela kama asipotoa hela ya matumizi kwa mtoto!



Bondia mkongwe Evander Holyfield anaweza kukabiliwa na kifungo jela kama asipotoa takriban $300,000 kama fedha za matumizi kwa mwanae.
Bondia huyo hajatoa fedha hizo kwa ajili ya mwanae wa kike Emani,18, tangu April 2010 alipoamriwa na mahakama kufanya hivyo.
Na sasa anadaiwa $372,097.40.
Msemaji wa Evander ameuambia mtandao wa TMZ kuwa hakuwa na taarifa kuhusiana na jambo hilo na kuongeza kuwa, “Holyfield ana uhusiano mzuri na binti yake.”
Hata hivyo ‘Upendo haulipi bili’. Toa hela!

Baada ya Fishcrab,producer Lamar aja na Filmatic



Producer na mshindi wa tuzo za Kili Lamar wa Fishcrab ameamua kuonesha kuwa si uandaaji wa muziki pekee anaouweza bali kamba yake ni ndefu zaidi ya hapo ilipomfikisha.
Mpishi huyo wa midundo ya ukweli nchini, amefungua kampuni mpya chini ya himaya yake ya Fishcrab iitwayo Filmatic.
Akiwa muongozaji mkuu na mchukua picha, mpaka sasa Lamar na timu nzima ya Filmatic ameshatengeneza video tano.
Jana kupitia ukurasa wa Twitter alisema Continue reading

Licha ya kwenda jela, pambano la dhidi ya Mayweather na Pacquiao lanukia



Juzi bondia Floyd Mayweather alijisalimisha mwenyewe jela huko Las Vegas kutumikia kifungo cha siku 87 kutokana na kosa la kumshambulia mpenzi wake wa zamani mbele ya watoto wao.
Hata hivyo hatua hiyo haijaathiri pambano linalongojewa kwa hamu kuliko yote kati yake na mfilipino Manny Pacquiao. Habari njema ni kuwa mabondia hao sasa hivi wanazungumza moja kwa moja.
Kwa mujibu wa mwalimu wa Pacquiao Freddie Roach pambano hilo linanukia.
“Golden Boy (promota wa Mayweather) na (Arum, promota wa Pacquiao) wanachukiana kiasi ambacho wameamua kukaa pembeni. Kwahiyo Manny na Floyd wameanza kuongea wenyewe, ” alisema Roach.
“Watagawana 40-40 na mshindi atachukua hela ya ziada. Kitu ambacho ni sawa sababu kila mmoja anasema atashinda.”

Wakazi aja na kanuni kumi za hela



Ukimuuliza Fid Q ni rappers gani anaowakubali zaidi Tanzania hawezi kukosa kumtaja Webiro Wasira aka ‘Wakazi’. Kama Fid kamkubali hatuna shaka kuwa uwezo wake si haba.
Jamaa anatokea pande za Ukonga, Dar es Salaam lakini kwa muda mrefu sana anaishi Chicago, Illinois nchini Marekani.
Katika ulimwengu wa Hip Hop wakazi ni mfalme wa kanda mseto (mixtape). Mpaka sasa ameshaachia mixtape tatu, MYU: Mixtape Ya Ukweli, MYU2 The Return of The Bilingual Beast na MYU3 Welcome To Heartbreak.
Jumapili hii amekuja na kanuni kumi za hela alizoziweka kwenye vina, ambazo ni hizi zifuatazo:
Continue reading

Wahu akanusha kumuimbia mumewe kwenye ‘Liar”



Mwanamuziki wa kike wa nchini Kenya Wahu amezikanusha story kuwa amemlenga mumewe kwenye wimbo wake Liar.
Kwa muda mrefu wapenzi wa muziki nchini humo wamekuwa wakihisi kuwa anayeambiwa ‘mwongo’ kwenye ngoma hiyo ni mume wake David Mathenge, aka Nameless, ambaye ni maarufu sana kwa mashabiki wa kike.

Katika interview aliyofanya na kituo cha radio cha Easy FM Wahu amesema kisa hicho ni cha kutunga.
“Kila mtu anaendelea kusema, aya, maze sema tu ukweli, you know. (The liar) ni uhusika wa kutunga lakini unaozungumzia mambo yanayotokea. Si unajua watu ni waongo,” alifafanua.
Wimbo huo kutoka kwa mshindi huyo wa tuzo za MTV, Wahu Kagwi umetengenezwa na producer maarufu

Tyrese: Nahitaji kufanya movie nyingine na Taraji



Unaikumbuka filamu maarufu sana ya Baby Boy (2001) aliyoigiza mwanamuziki Tyrese, rapper Snoop Dogg na muigizaji maarufu Taraji P Henson?
Katika filamu hiyo Tyrese ameigiza kama Jody (20) anayeishi na mama yake Juanita. Tyrese ameigiza kama mtoto wa mama fulani ambaye haoneshi dalili ya kuwa mtu mzima na kukabiliana na majukumu kama baba baada ya kumzalisha mpenzi wake Yvette (Taraji P. Henson) mtoto wa kike aitwaye Peanut.
Kwa muda mrefu watu wamekuwa wakisubiri sana ujio mpya wa filamu nyingine itakayowakutanisha wawili hao. Leo (June 2) Tyrese kupitia Twitter ameonesha kuwa yeye pia ana hamu ya kukutana na Taraji. “I need to do another movie with this woman …. Fast … Where is my baby.?” Ametweet akiambatanisha picha waliyopiga pamoja.
Tweet hiyo inatupa maswali mengi hasa anapoandika’ Fast’ kwasababu tunajua kuwa awamu ya sita ya filamu maarufu ya Fast and the Furious ambayo Tyrese yumo kwenye zote tano zilizopita, huenda Taraji akaonekana humo pia! You never know!

Mwezi July mwaka jana Tyrese alitweet pia kwa kuandika, “Official.. Me and my girl Taraji are doing another classic together soon.!! John Singleton will be directing us. And it’s not BB2.”
Vyovyote itakavyokuwa, Taraji na Tyrese wanapendeza sana kuwa kwenye movie moja.

Photos: Maandalizi ya show ya Kili Music Awards winners Tour Dar


Saturday, June 2, 2012

LINAH-AWASILI DAR-ES-SALAAM LEO BAADA YA KUMALIZA TOUR YAKE YENYE MAFANIKIO USA…TAYARI KWA SHOW YAKE YA MISS MWANZA

Posted  on June 2, 2012 by  amran
Linah katika pozi la Finally niko nyumbani baada ya ziara ndefu yenye mafanikio Marekani.
Linah akiwa na mama yake na mdogo wake katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Daressalaam Tanzania.
Bi Linah alipopokelewa kwa shangwe na ndugu yake Neyounce.

Home sweet Home Linah mwenye furaha kubwa baada ya kufika nyumbani kwake.

JK AKUTANA NA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA IRAN NA MJUMBE WA RAIS WA BURUNDI IKULU DAR ES SALAAM

Posted  on June 2, 2012 by amran Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpokea Ikulu jijini Dar es salaam Mei 30, 2012 Mjumbe maalumu kutoka serikali ya Burundi, Mh Martin Nivyabandi, ambaye ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii wa nchi hiyo. Kati ni Balozi wa Burundi nchini Tanzania.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran Mh Muhammad Reza Rahimi Ikulu jijini Dar es salaam Mei 30, 2012. Kiongozi huyo yuko nchini kwa ziara ya kikazi.(PICHA NA IKULU)

Hasheem Thabeet launches Basketball Clinic in Dar

Sauti Sol to Perform Alongside Alanis Morisette and Janelle Monae

3
 

Kenya’s leading afro fusion boy band Sauti Sol are set to perform at the Czech Republic’s BIGGEST music festival of the year, the Colours of Ostrava from the 12th to the 17th of July 2012.
News coming from Nairobi says Sauti Sol are set to perform alongside other established artistes from across the globe including America’s Alanis Morisette, Sea and Air and Janelle MonĂ¡e.
The group which also featured Tanzania’s rap crooner AY in their hit song collabo “I don’t wanna be alone” track,has been very active this year on the international circuit, with a variety of acclaimed appearances at the South by South West Festival in Austin Texas USA and at the Festival on the Niger in Mali earlier this year. Continue reading

Wednesday, May 30, 2012


Video ya ‘No Church in the Wild’ ya Kanye West na Jay-Z yatoka ikiwa na ujumbe mzito

Hatimaye video ya wimbo mpya wa Kanye West na Jay-Z, “No Church in the Wild” jana imetoka. Video hiyo inawaacha mashabiki na ujumbe mzito hata kama nguli hao wawili hawaonekani kwenye video. Kwa mujibu wa MTV uamuzi huo wa Kanye … Continue reading

Facebook kuanza kutengeneza simu kama iPhone!!


Theluthi ya watumiaji wa simu wako tayari kununua simu ya Facebook (smartphone) na asilimia 73 wanadhani wazo la mtandao huo kuwa na simu zake ni zuri.
Habari za simu hiyo zimeibuka wiki hii huku vyanzo vikidai kuwa Facebook imemwajiri engeener wa zamani wa Apple kutengeneza simu ‘rasmi’ ya Facebook.
Sio mara ya kwanza kwa simu za Facebook kuingia sokoni.
Mtandao huo wa kijamii uliwahi kuingia ubia na makampuni ya INQ na HTC kutengeneza simu za Facebook zikiwemo simu zilizowekewa button ya ‘Like’ ndani.
Simu hiyo inasemekana itakuwa tayari kuzinduliwa rasmi mwaka ujao.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na MyVoucherCodes kwa kuhoji watu 968, asilimia 32% wamesema watainunua ikiwa tayari.
Asilimia 57 wamesema wanaamini simu hizo zitakuwa na bei nafuu kuliko iPhone.
Baada ya iphone kupata ushindani mkubwa kutoka kwa Samsung Galaxy, Facebook kuwa mpinzani mwingine mwenye nguvu? Yetu masikio.

Will Smith: Nina bahati Jada kuwa mke wangu


Will Smith amemsifia mke wake Jada Pinkett kwa kuifanya familia yake kuwa pamoja.
Muigizaji huyo wa Men In Black III na mke wake muigizaji wa series ya Hawthorne wana miaka 17 tangu waoane licha ya hivi karibuni kuwepo na fununu kuwa ndoa yao ipo matatani kuvunjika. Continue reading
Posted in Will Smit


AY hulipwa kila wimbo wake unaposikika Big Brother


Kuna faida nyingi mno za msanii anapotambulika kimataifa ambapo moja kubwa ni show nyingi za nguvu zinazomwijia kila kukicha.
AY aliligundua hilo mapema ndo maana hakuwa bahili kusafiri nje ya nchi kufanya collabo na wasanii wa kimataifa na kuingia gharama kubwa kufanya video.
Juzi tu ametoka Johannesburg kufanya video iliyochomoa zaidi ya milioni 31 kutoka kwenye akaunti yake.
Hivyo usishangae kuambiwa kuwa kila usikiapo wimbo wake umechezwa Big Brother Africa, kuna hela inaingia kwenye akaunti yake bila matatizo.
Jana wimbo wake Leo aliofanya na Prezzo ambaye ni mshikaji wake wa karibu, ulikuwa ukipigwa, na rais huyo wa Cash Money Brothers wa Kenya alikuwa akiiufurahia.
Lakini kuna mtu ambaye alitaka kujua zaidi kama AY anapata chochote kwakuwa hiyo si mara ya kwanza wimbo wake kuchezwa, “hivi kuna hela unalipwa kwa nyimbo zako kupigwa @BigBroAfrica?” ambapo AY alijibu “Yes baus.”
Kwa Bongo hiki ni kitu kigeni kwakuwa bado kuna mjadala mkubwa kati ya wamiliki wa radio na TV kuhusu kuwalipa wasanii kila wanapocheza nyimbo zao (radio/TV royalties) lakini kwa wenzetu hii ni njia mojawapo inayowaingiza pesa wanamuziki.

Filamu ya The Avengers’ yafikisha mauzo ya dola bilioni 1.3 duniani kote


Inaonekana The Avengers itavuka matarajio kwa mara nyingine tena.
Filamu hiyo sasa inatishia nafasi ya tatu inayoshikiliwa na filamu ya mwisho ya Harry Potter katika orodha ya filamu zilizoingiza fedha nyingi zaidi.
Harry Potter and the Deathly Hallows, Part 2 imeingiza dola bilioni 1.328 duniani kote na kuwa nyuma ya filamu za James Cameron ambazo ni Titanic inayoshikilia nafasi ya pili na Avatar inayoshikilia nafasi ya kwanza.
Kwa mujibu wa jarida la Forbes, The Avengers sasa imeshaingiza dola bilioni 1.305 duniani kote kwa kuoneshwa kwenye majumba ya sinema.
Inaonesha pia kuwa The Avengers iliyozinduliwa April 11 mwaka huu duniani kote, itaipita The Dark Knight inayoshikilia nafasi ya tatu kwa kuingiza fedha zaidi nyumbani (Marekani).
Kwa sasa The Avengers iliyotayarishwa kwa bajeti ya dola milioni 200, imeshaingiza dola milioni 513.6 kutoka kwenye soko la nyumbani, ambazo ni pungufu ya dola milioni 19.7 tu zilizoingizwa na The Dark Knight nyumbani.
Haijulikani mapato ya The Avengers yatafika kiasi g