amreezle

amreezle

Thursday, April 26, 2012

RAIS KIKWETE AWAONGOZA WATANZANIA KWENYE SHEREHE ZA MUUNGANO.

Postd on April 27, 2012 
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia wananchi wakati alipokuwa akiingia katika uwanja wa uhuru jijini Daresalaam kuongoza maadhimisho ya miaka 48 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar alhamisi asubuhi.
Rais Kikwete akisalimiana na Mama Maria Nyerere katika uwanja wa Uhuru jijini Daresalaam
(Picha wa hisani ya Michuzi)

HALAIKI YA WANAFUNZI YAPAMBA SHEREHE ZA MUUNGANO WA TANZANIA

Posted on April 27, 2012 

Hawa si wanafunzi wa jamhuri ya kikomunisti ya China bali ni wanafunzi wa Tanzania wakifanya vitu wakati wa sherehe za muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwenye uwanja wa uhuru Daressalaam Tanzania.
Halaiki ya wanafunzi wapatao 1,727 kutoka shule za msingi mbalimbali Tanzania bara na visiwani waliipamba vizuri sherehe ya maadhimisho ya miaka 48 ya Muungano wa Tanzania yaliyofanyika alhamisi katika viwanja vya Uhuru jijini Dar es Salaam.
Kati ya wanafunzi hao, ni wanafunzi 727 ambapo 500 wanatoka Tanzania bara, 200 Tanzania visiwani na 27 ni mahodari wa kucheza sarakasi ambao waliingia uwanjani na kutengeneza maumbo mbalimbali pamoja na kuimba wimbo maalumu uitwao Uamuzi wa Busara.
Katika maadhimisho hayo Mgeni rasmi alikuwa ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Jakaya Mrisho Kikwete na kauli mbiu ni “Shiriki kikamilifu katika Sensa na mchakato wa Mabadiliko ya Katiba”.Kwa hisani ya full shangwe.

WAPINZANI WA SIMBA WAMEWASILI DAR

Posted on  April 27, 2012
Wakati msafara wa watu 30 wakiwemo wachezaji na viongozi wa timu ya soka ya Al Ahly Shandy ya Sudan ukiwasili nchini leo kwa ajili ya kukwaana na Simba, mgeni rasmi katika mechi hiyo anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.
Timu hizo zitakwaana Aprili 29 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa 16 bora ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF).
Akizungumza mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Kimataifa wa Mwl. JK Nyerere, kocha mkuu wa Al Ahly Kouk Mohammed aliiambia mamapipiro blog kwamba mchezo huo uantarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwani Simba ni timu nzuri.
Alisema anaifahamu Simba kama moja ya timu mahiri barani Afrika sambamba na kuwa na uzoefu wa kucheza michuano ya kimataifa hali ambayo itawafanya wawe makini zaidi pindi watakaposhuka dimbani.
Hata hivyo kocha huyo raia wa Tunisia alisema kwamba huenda wakaathiri kidogo na hali ya hewa ya Tanzania kutokana na kuwa tofauti na Sudan ingawa watajitahidi kukabiliana nayo.
Kikosi cha Al Ahly kinaundwa na wachezaji watano wa kimataifa wakiwemo wawili kutoka Nigeria , mmoja kutoka Mali na mwingine kutoka Mali huku wachezaji wawili wakiichezea timu ya Taifa ya Sudan .
Al Ahly wanakutana na Simba baada ya kuitoa Ferroviario ya Msumbiji kwa jumla ya mabao 3-0, huku Simba iliitoa Es Setif ya Algeria huku Simba ikibebwa na bao la ugenini baada ya nyumbani kushinda 2-0 kabla ya kwenda kufungwa 3-1.
Katika hatua nyingine tiketi kwa ajili ya kushuhudia mpambano huo zinatarajiwa kuanza kuuzwa leo katika vituo tofauti jijini Dar es salaam huku waamuzi wa mchezo huo kutoka Swaziland Nhleko Simanga Pritchard, Mbingo Petros Mzikayifani,Sibandze Thulani, Fakudze Mbongiseni Elliot na Kamishna wa Kayijuga Gaspard wa Rwanda wanatarajiwa kuwasili leo.
Katika kujiandaa na mchezo huo, Simba imepiga kambi eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam ambapo kocha mkuu wa Simba Mserbia Milovan Cirkovic amejinasibu kushinda mchezo huo ili kujiweka katika mazingira mazuri kwenye mchezo wa marudiano utakaopigwa wiki mbili zijazo katika jiji la Shandy , Sudan .
Chanzo: www.Bongostaz.blogspot.com

WAZIRI MAIGE ASEMA ALILIPA DOLA 410,000 LEMBELI APINGA, ASEMA ALIINUNUA KWA DOLA 700,000 TASLIMU

Posted on April 27, 2012

SIKU chache baada ya gazeti la Mwananchi kuripoti taarifa za uchunguzi kwamba kuna mawaziri wawili ambao wamenunua nyumba mbili zenye thamani ya Sh1.8 bilioni, mmoja wa mawaziri hao, Ezekiel Maige wa Maliasili na Utalii ameibuka na kukiri.Maige aliliambia gazeti hili jana kuwa nyumba yake hiyo iliyoko Mbezi Beach, Dar es Salaam, ameinunua kwa Dola za Marekani 410,000 (takriban Sh656 milioni) ambazo anadai kuwa ni mkopo kutoka Benki ya CRDB.
Hata hivyo, wakati Waziri Maige akieleza kuwa nyumba hiyo ina thamani hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli amedai kuwa taarifa alizonazo ni kwamba ilinunuliwa kwa fedha taslimu Dola 700,000 za Marekani (takriban Sh1.1 bilioni).Kusoma zaidi bofya Read more »

Waziri akiri kununua nyumba ya mamilioni

Posted on April 26, 2012 
Waziri wa maliasili na utalii Tanzania Ezekiel Maige.
Siku chache baada ya gazeti la Mwananchi kuripoti taarifa za uchunguzi kwamba kuna mawaziri wawili ambao wamenunua nyumba mbili zenye thamani ya Sh1.8 bilioni, mmoja wa mawaziri hao, Ezekiel Maige wa Maliasili na Utalii ameibuka na kukiri.Maige aliliambia gazeti hili jana kuwa nyumba yake hiyo iliyoko Mbezi Beach, Dar es Salaam, ameinunua kwa Dola za Marekani 410,000 (takriban Sh656 milioni) ambazo anadai kuwa ni mkopo kutoka Benki ya CRDB.
Hata hivyo, wakati Waziri Maige akieleza kuwa nyumba hiyo ina thamani hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli amedai kuwa taarifa alizonazo ni kwamba ilinunuliwa kwa fedha taslimu Dola 700,000 za Marekani (takriban Sh1.1 bilioni).
Awali, habari zilizolifikia gazeti la Mwananhgi zilieleza kuwa Waziri Maige alinunua nyumba hiyo kutoka kwa Kampuni ya Savana Real Estate. Kusoma zaidi bofya Read more »

SIKU LINAH ALIPOWAPA RAHA WATU WA COLUMBUS OHIO

Posted  on April 26
Linah akifanya vitu vyake katika ukumbi wa Monkey’s Bar Columbus Ohio.Jumamosi hii April 28 atazazamua New York New York.
Linah na Aj jukwaani.
Linah akipewa love na mashabiki wa Ohio.
Wapenzi wa Linah Ohio wakiselebuka.
Bi.Janita wa pili kulia kwa raha zake akiselebuka na mashabiki wengine wa Lina jijini Ohio. Kwa picha zaidi bofya Read more »

No comments:

Post a Comment