amreezle

amreezle

Thursday, October 13, 2011

MAKOSA KATIKA MOVIE YA TITANIC (1997)

MAKOSA KATIKA MOVIE YA TITANIC (1997)



MAKOSA KATIKA MOVIE YA TITANIC
1.Kuna scene Jack anamtishia  Rose kuruka baharini,ile haikuwa bahati bali ni ziwa  Wissota, ni man-made lake ,ambapo karibu na hilo ziwa ndio Jack alikulia.Hili ziwa lilijazwa maji mwaka 1918 baada power company kujenga bwawa katika mto Chippewa , hii ilikuwa ni miaka sita baada ya Titanic kuzama
2.Wakati Jack na Rose wanazama na meli kuna mtu alikuwa ameshkilia flagpole,huyu mtu life jacket yake ilikuwa inaoneka katika katika shot moja na kupotea katika shot nyingine,kitu ambacho hakikutakiwa kuwapo
3.Cameraman:.Wakati Jack anakuja katika mlango wa watu wa first clack katika meli Cameraman aliekuwa akishoot movie alionekana katika kiyoo
4. Wakati Rose na Jack wanamkimbia Cal ambae alikuwa akiwashoot kwa risasi ktk dinning room,sakafu ya meli ilikuwa imebinuka kuashiria kwamba meli ilikuwa ikizama but katika scene ilofata walipokuwa wanakimbia ktk level ya chini ya meli,sakafu ilikuwa level
5.Mistake Wakati Rose anakimbia huku na huko akitafuta mtu wa kwenda mnasua Jack,anakutana na mtu na kumuomba life Jacket ya ziada alokuwa ameishika,anakerwa na response ya yule mtu na kumtandika,ukiweka slow motion utagundua katika sehem ya uso alopigwa yule mtu tayari ilikuwa ikitoka damu hata kabla hajapigwa
6.Baada ya kupigwa risasi katika na Cal, Rose na Jack wanakimbia chini huku maji yakiongezeka. Rose anaonekana amevaa sneakersnyeupe, lakini baada ya dakika mbili baadaye anaonekana amevaa period shoes.this is rediculous

7.Mistake Wakati meli inakaribia kuondoka bandarini, kundi kubwa la watu linaonekana likiwapungia mikono ya kwaheri . Katika shots zilizofuata, unaweza kuona Jack na marafiki zake wakicheza karata ndani ya baa. Kama ukiangalia kwa dirisha huwezi kuona mtu yeyote bandarini. ila cha kushangaza ktk shot ilofata Jack alipokuwa anaondoka ktk pub crowd ya watu inaonekana bandarin
8.Mistake  wakati Jack na Rose wanakimbizwa na Cal dinning room taa na vifaa vya wachukua movie vilikuwa vinaonekana kupitia dirisha,kama ukiangalia kwa umakini
9.Mistake Makosa ya makusudi: Wakati Jack anamchora Rose mkono unaoonekana kwa karibu unaonekana dharihi ni wa mtu mwenye umri mkubwa kuliko Jack,ni mkono wa James Cameron

Release date

Filming Dates:16 September 1996 - 23 March 1997
Copyright Holder:-Paramount Pictures Corporation
Twentieth Century Fox Film Corporation
 USIYOYAJUA KUHUSU MOVIE YA TITANIC
1.Katika hatua za mwanzo za production hii movie waliiita  ”Planet Ice”.
2.Ilikuwa ndio movie iloingiza pato kubwa katika box office history,ikiinngiza takriban US$1.8 billion but baadae ilipitwa na  Avatar. Hizi filam mbili zote ziliongozwa na  James Cameron
3.Mwanzoni budgeted ya movie ilikuwa $135,000,000, but schedule iliporefushwa kwa miezi miwili zaidi waliiomba kampuni ya Paramount Pictures kuongeza $65,000,000
4.Baada ya kumaliza Terminator 2: Judgment Day, James Cameron alijiwa na wazo baada ya kuangalia movie ya  A Night to Remember.Alikaa chini na kufanya research ya miaka mitano kuhusu meli ya  Titanic na yaliyoisibu

5.Kate Winslet  ni mmoja kati ya actors walokataa kuvaa nguo ya kuogelea katka scene ya majini,matokeo yake alipata pneumonia
6Movie ilikuwa namba moja katika U.S. box office kwa wiki 15 mfululizo,kuanzia 19 December 1997 mpaka 2 April 1998.
7.Mkono ulokuwa ukionekana ukimchora Roseio waLeonardo DiCaprio‘s, ila ni wa director James Cameron‘s. Katika editing baadae, Cameron, ambae anatumia mkono wa kushoto,walitumia technique ya kuipindua shot kwa kiyooo(hapa watu wa editing ndo wanaelewa zaidi)ili ionekane ni mchoraji alikuwa anatumia mkono wa kulia,kama DiCaprio.
8.Hii ni movie ya kwanza kuwa filmed katika Fox Studios Baja.
9.Katika scene ambayo wazee wawili wapenzi wanakumbatiana kitandani wakiwa tayari kufa pamoja wakati meli inazama na maji yashaanza ingia chumbani kwao na kuanza sambaa chini ya kitanda,mtunzi hapa anawatumia hwa wahusika wawili kuelezea kilichotokea kwa wamiliki wa Macy’s department store ya mjini New York; Ida and Isidor Strauss.Hawa walikuwa ni wapenzi wawili walokufa katika Titanic in real life. Ida alikuwa offered a seat on a lifeboat but alikataa ili akae na mme wake,Ida alitamka maneno haya, “As we have lived together, so we shall die together.”Scene inayoelezea hili tukio ipo moment, ila ilikatwa,unaweza iona katika Special Collecters DVD
10.Hii ndio the expensive movie kuwa filmed katika karne ya 20
11.Katika movie,wakati engine master anasema “All ahead full,” kuna mtu aliskika akipiga yowe , “All ahead full!” katika background. Hiyo ilikuwa sauti ya director James Cameron
12.James Cameron ndo alichora picha zote katika movie
13.Baada ya kujua atasmama uchi mbele ya  Leonardo DiCaprio, Kate Winslet aliamua kuwekaa aibu pembeni,walipokutana kwa mara ya kwanza ali smile kidogo na kuangalia pembeni
14.Christian Bale aliomba nafasi ya kucheza katika moja ya nafasi muhim ila James Cameron alikataa,hakuwa anataka waigizaji wawili wa kiingereza wacheza nafasi muhim zote katika hii movie
15.Gwyneth Paltrow alikuwa akiimendea nafasi ya kucheza kama ROSE but  Kate Winslet ndiye alipata
16.Hii ilikuwa ni  film ya kwanza kuwa released katika (DVD/VHS) wakati bado inaoneshwa katika nyumba za cinema
17.Mwishoni mwa movie wakati  Rose anakutana na Jack ktk Grand Staircase, muda ulokuwa unaonekana katika saa ya ukutani ndo muda halisi meli yenyenyewe ya Titanic ilipozama
18.Hii ilikuwa ni film ya kwanza James Cameron  kudirect bila ya neno ”nuclear weapons” kutotajwa
19.James Cameron alikutana na mke wake wa tano, Suzy Amis, katika hii  film. Of all his marriages, na kak ndoa zote za jamaa hii ndo ilidumu mda mrefu.
20Nicole Kidman, Madonna, Jodie Foster, Cameron Diaz and Sharon Stone hawa wote walikuwa wakifkiriwa kucheza part ya Rose.
21.3-D ya hii movie itatolewa April 2012, ikumbukwe huo ulikuwa ni mwezi ambao meli yenyewe ya the RMS Titanic ilianza safari miaka  100 ilopita
22.Hii ilikuwa ni movie ya kwanza kuwa na budget ya $200,000,000.
23.Sehem kubwa ya waigizaji walikuwa wakiruka baharini maji yake yalikuwa na kina cha 3 feet deep.
24.Katika  scene ambayo maji yanapiga milango kwa nguvu , James Cameron alisema Galoni  40,000 za maji zilikuwa hazitoshi kujaza korido zile,akaagiza mara tatu yake
25.James Cameron alikuwa mbishi ku kuingiza nyimbo yoyote katika hii movie.Mtunzi James Horner akiwa na lyricist Will Jennings pamoja na Céline Dion waliandika nyimbo ya “My Heart Will Go On” kwa siri kubwa na kurecord demo tape, then wakaipresent kwa Cameron. Nyimbo ilishinda Oscar.
26.Gharama ya hii movie($200) ni kubwa kuliko gharama ya meli halisi ya Titanic($150 million)
27.James Cameron alikatwa $8 million kama sehem ya salary yake baada ya studio kukerwa na fact kwamba movie ilienda over budget
NOTE:
When exactly did the Titanic sail?

The ship left Southampton, England on Wednesday 10 April 1912 and took on more passengers at Cherbourg, France and Queenstown, Ireland (now called Cobh) later that day. On Sunday 14 at 11:40 p.m. (ship time) she struck an iceberg 400 miles (650 km) south of Newfoundland, and went under at 2:20 a.m.

No comments:

Post a Comment