amreezle

amreezle

Thursday, September 29, 2011

MUONEKANO MARIDHAWA....!

Sifa moja ya miji mingi mikubwa duniani huwa ni pamoja na kuwa na majengo,ma-sanamu au kitu kingine chochote kikubwa ambacho hutumiwa kama kitambulisho au alama rasmi ya jiji husika.Kwa jiji la London lililopo nchini Uingereza, Tower Bridge(pichani) ni mojawapo ya “landmark” muhimu za jiji hilo.

Unaweza kusoma kuhusu historia ya Tower Bridge kwa kubonyeza hapa.Lakini wengi nadhani tungependa zaidi kusikia kutoka kwa wenzetu wanaoishi London au nchini Uingereza kuhusu umuhimu wa Tower Bridge kwa jiji la London.Tunakaribisha pia picha kama hizi kutoka katika majiji mengine duniani ambako tuna hakika watanzania wametapakaa huko.Hii yote ni katika kusaidiana katika kufunguana macho.Na je kwa jiji letu la Dar-es-salaam,tunaweza kusema “Askari Monument” ndio kitambulisho chetu rasmi?

No comments:

Post a Comment